Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Ado Shaibu Ado (1 total)

MHE. ADO S. ADO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kuniona. Kwa vile tatizo hili la tembo kuvamia vijiji na kuharibu mazao, kuuwa binadamu ni tatizo kubwa sana katika Jimbo la Tunduru Kaskazini na Wilaya ya Tunduru kwa ujumla wake. Ambapo kwa msimu wa kilimo wa 2025/2026 peke yake jumla ya waathirika 1791 wameharibiwa mazao yao na askari wa vijiji mpaka sasa wako 23 tu. Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa waathirika wote na kuongeza idadi ya askari wanyamapori wa vijiji (VGS)?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeshaweka fedha na zimeshaingia na sasa tunafanya utaratibu wa kulipa kupitia mfumo. Kilichochelewesha ilikuwa tunalipa manual, unaenda kijijini unaenda kulipa, pengine unaenda kulipa milioni tano unatumia gharama ya milioni nne, lakini kwa sasa tunatumia mfumo na mfumo huu umetuwezesha. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira hawa watu wetu watapata malipo yao.