MHE. ENOCK Z. KOOLA aliuliza :-
Je, lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwa ajili ya kilimo cha chakula katika Jimbo ya Vunjo?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji katika Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo Jimbo la Vunjo. Kwa mwaka 2025/2026, miradi mitano inaendelea kutekelezwa katika Jimbo la Vunjo ikihusisha mradi wa ujenzi wa Skimu ya Mawala wenye ukubwa wa hekta 2,500 unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 4.1.
Mheshimiwa Spika, vilevile, miradi minne imepangwa kutekelezwa katika mwaka wa fedha ujao wa 2026/2027 inayojumuisha skimu nne za Mananga, Ndekambeko, Masaera na Masaga ambapo mkandarasi ameshapatikana.