Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Joseph Enock Tama (1 total)

MHE. JOSEPH E. TAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Igwisi katika Jimbo la Kaliua?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kaliua kwamba pamoja na yeye tayari tumeshawasilisha andiko kuhusu hili ombi la fedha kutoka Hazina. Kwa hiyo, kituo cha afya cha kimkakati katika Jimbo la Kaliua, kwa confidence kabisa nimwambie Mheshimiwa Mbunge awaambie wananchi kwamba tunakwenda kukijenga na kianze kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.