MHE. SHADYA HAJI OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niendelee kuipongeza Wizara hii kwa mazuri ambayo wanayafanya na mengi tukiwa tunayashuhudia. Niende moja kwa moja kwenye swali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vikundi vingi vya akina mama vinakufa kwa sababu ya mitaji pamoja na masoko ya uhakika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuunganisha wanawake hawa na masoko ya EAC na SADC badala ya kutegemea masoko ya ndani?
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE WA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru sana Mheshimiwa Shadya kwa pongezi, lakini kuona kwamba Serikali inaunganisha haya makundi ya wanawake na masoko ya nje kama nilivyotoka kujibu swali langu lile la kwanza kwa mwuliza swali la msingi. Tayari tunafanya, ila niseme kwamba tunapokea huu ushauri ili kuongeza kasi ya kuona tunawapeleka makundi ya wanawake kwenye masoko ya nje zaidi.