MHE. MUHSIN HAJI USSI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha wale vijana ambao wapo vijijini hawana smartphone na hawana uwezo wa ku-access mitandao ya kijamii, wanaweza kufikiwa kwa haraka kuweza kupata taarifa husika juu ya uwepo wa fursa hizi kwa vijana Tanzania? Nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA NA MAHUSIANO (MHE. RAHMA R. KISUO) K. n. y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA: Mheshimiwa Naibu Spika, hili nimelijibu pia, kwenye swali la kwanza la nyongeza la Mheshimiwa Juwakali. Kwa wale ambao hawataweza kupata access ya social media, tunaweza kutoa elimu kupitia makongamano na maadhimisho mbalimbali. Vilevile baadhi ya fursa zimekuwa zikibandikwa katika mbao mbalimbali za matangazo za watendaji kata na vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.