MHE. BARAKA A. U. MWAMENGO aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Ibanda – Kiwira Port kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Baraka Ulimboka Mwamengo, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba wa ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Ibanda – Kajunjumele – Kiwira Port yenye urefu wa kilometa 28 ulisitishwa baada ya mkandarasi aliyekuwepo kushindwa kutekeleza mradi kwa mujibu wa mkataba. Taratibu za manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi mwingine zinaendelea. Ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami utaanza baada ya taratibu za manunuzi kukamilika.