Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon William Kafiti Kafiti (2 total)

MHE. KAFITI W. KAFITI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, bado sisi kama Mwanza na kama wakazi wa Jimbo la Ilemela, tunahitaji kujua huo upembuzi yakinifu utakamilika lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ukamilishwaji wa uwanja huu...
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kafiti Mbunge wa Ilemela alikuwa anajaribu kukazia hoja ile ile ya uwanja wa ndege na kimsingi yeye pale kwake hoja kubwa ambayo anaizungumzia ni upande wa fidia au namna ya kuweza kuondoa wananchi wa pale. Serikali ina dhamira ya kuufanya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa. Ili uweze kuwa na sifa hizo, lazima kama kuna wavamizi waondolewe. Kwa hiyo, nimwombe tu awe na subira, tutamilisha muda siyo mrefu tutaanza kufanya kazi.
MHE. KAFITI W. KAFITI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniruhusu kuuliza swali la nyongeza. Itakumbukwa tarehe 2 Juni, 2023 Wizara ya Utamaduni na Michezo mliomba eneo katika Wilaya ya Ilemela eneo la North Buswelu kwa ajili ya kuanzisha kituo cha ufundishaji wa michezo, lakini mpaka sasa hakuna kitu kinachoendelea. Je, ni lini Serikali itatimiza maombi yake juu ya eneo hilo?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikijibu swali la Mheshimiwa Kafiti, Mbunge wa Ilemela ni kwamba kweli Serikali tarehe 2 Juni, 2023 iliandika barua kwa ajili ya kuomba eneo kutengeneza Center for Sports Excellence pale Ilemela na mpango ule haujafa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilijibu wakati najibu kwenye swali la msingi la Mheshimiwa Amari, kwa sasa tumejielekeza kwenye ujenzi wa miundombinu itakayotumika kwa ajili ya mashindano ya AFCON. Pia Serikali inaanzisha Taasisi ya Sports Infrastructure Management Agency ambayo kazi yake itakuwa pamoja na mambo mengine kutambua, kujenga, kukarabati na kusimamia, kwa maana ya kuendesha maeneo mbalimbali ya michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Ilemela halijatoka kwenye mipango ya Serikali, na nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Kafiti aendelee kuwa na Subira, litafikia muda wake na litafanyika tutakapomaliza programu hii ya ya AFCON.