Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Ali Vuai Khamis (1 total)

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga kituo cha Polisi katika Kijiji cha Matemwe Jimbo la Mkwajuni Unguja kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo katika eneo hilo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, kumjibu swali Mheshimiwa Ali Vuai Khamis, Mbunge wa Mkwajuni, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la Matemwe Jimbo la Mkwajuni, hakuna sehemu iliyotengwa rasmi kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Polisi. Napenda kutumia fursa hii kupitia Bunge lako Tukufu, kumshauri Mheshimiwa Mbunge pamoja na Kamisheni ya Ardhi Zanzibar kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kutenga eneo kwa ajili Kituo cha Polisi Matemwe, ili Serikali iweze kutenga fedha kutoka kwenye bajeti yake kwa ajili ya kujenga kituo hicho cha Polisi.