Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Mary Daniel Surati (1 total)

MHE. MARY D. SURATI: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo ameendelea kuyatoa. Pia nilikuwa ninaomba wananchi wa Jimbo la Seregenti wanaomba kufahamu, ni lini Serikali itaanza kutoa fidia stahiki inayoendana na hasara wanazopata wananchi wanaoathirika na Wanyamapori? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, Serikali inatoa fidia stahiki kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizowekwa. Kwa hiyo, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi hawa wataendelea kupata fidia ambazo wanastahiki, na kwa sasa hakuna mtu yeyote ambaye atakosa haki yake ya msingi.