Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Zainabu Athuman Katimba (1 total)

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, Barabara ya Jaribu – Mpakani, Kivinje – Nanjache yenye urefu wa kilometa 32 ujenzi wake umesimama, mkandarasi hayupo site na muda wa ujenzi ulishakwisha. Ni nini kauli ya Serikali juu ya kadhia hii?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): Mheshimiwa Spika, ninaomba nitumie nafasi hii kumkumbusha Meneja wa TARURA Mkoa wa Pwani pamoja na Meneja wa TARURA ngazi ya Wilaya waweze kufanya ufuatiliaji wa karibu kabisa ili waweze kujua changamoto ni nini ambayo inafanya mkandarasi asiwepo site, lakini waweze kuamua changamoto iliyojitokeza. Wawasiliane na sisi kama kuna changamoto ambayo iko juu ya uwezo wao ili tuweze kuikwamua barabara hii iweze kujengwa na mkandarasi arudi site. (Makofi)