MHE. PROF. PIUS Z. YANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Hata hivyo, kwa kuwa taaluma ya teknolojia ya TEHAMA sasa hivi ni taaluma ya msingi sana katika maendeleo ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Serikali kwamba ujenzi wa chuo hicho uweze kupata kipaumbele. Hii itawezesha kwanza kunufaisha vijana ambao wakipata elimu hiyo wataweza kujiajiri kwa sababu ya ile elimu waliyoipata. Pia, hiyo itasaidia kusukuma gurudumu la maendeleo kwa kutumia teknolojia ya maendeleo vijana wetu watakuwa wamepata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa misingi hiyo basi, ombi letu ni kwamba, Serikali ione jinsi gani iweze kupata uwezeshaji wa ujenzi wa hicho chuo, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza Profesa, amekuwa akilifuatilia suala hili kwa karibu kwa Mheshimiwa Waziri na pia kwangu. Hii inaonyesha kwamba ana hamasa kubwa ya masuala ya teknolojia ya Habari, na Wananchi wa Buhigwe pia wana hamasa hiyo. Nimhakikishie kwamba ombi lake tumelipokea, na tutatoa kipaumbele kikubwa katika ukamilishaji wa chuo hicho.