MHE. HAIDERALI H. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana. Ninataka kujua, ni lini Hospitali ya Manispaa ya Mpanda itapata jengo la emergency?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye majibu ya awali, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Hospitali ya Mpanda nayo imo katika mpango wa zile hospitali 105 ambazo tumeshatenga bajeti katika mwaka wa fedha 2026/2027, jumla ya shilingi bilioni 52.25, ambazo tutazielekeza katika kukamilisha baadhi ya miundombinu muhimu.
Mheshimiwa Spika, ni kweli jengo la emergency ni muhimu sana kwa sababu linatoa huduma kwa wakati na baadhi ya wagonjwa huishia tu kutibiwa emergency na kwenda nyumbani. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa jengo hili muhimu.