Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Mwenyekiti, natangulia kumshukuru Mhashimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwekeza miradi mikubwa ya mawasiliano ya simu za mkononi kupitia maradi wa minara 1,494 (758 plus 636). Nakupongeza Mheshimiwa Waziri Jerry Silaa na Naibu wako Mheshimiwa Maryprisca Mahundi kwa kazi nzuri mnazozisimamia katika Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati nilipoingia madarakani na kuwa Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini jumla ya vijiji 22 havikuwa na mawasiliano ya simu za mkononi. Ndani ya miaka minne jumla ya vijiji 13 vimefikiwa na huduma za mawasiliano ya simu za mkononi. Jumla ya vijiji vinne vya Nandete, Mwengei, Chapita na Pungutini vilifikiwa na mawasiliano ya simu za mkononi ya minara ya TTCL ya 3BG mwezi Agosti, 2021. Minara na Madishi ya GB4 na 5 ya Tigo na Airtel katika vijiji vya Kandawale/Namatewa, Kipindimbi, Mkarango na Chumo. Minara hi imeongeza mawasiliano ya simu za mkononi katika vijiji kumi na vitatu. Aidha ipo miradi inayoendelea katika vijiji ya ujenzi wa minara ya TTCL na Tigo. Vijiji hivyo ni MT Kimwaga (Narayan), Miumbu/Mtyalambuko, Zinga Kibaoni (Nambunju), Marendego, Kandawale, Miguruwe/Mtepela na Ingirito. Miradi hi imepangwa kukamilika mwishoni kwa mwezi Mei, 2025. Itakapokamillika jumla ya vijiji 18 vitakuwa vimefikiwa na mawasiliano ya simu za mkononi ndani ya kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan na vitabaki vijiji vinne vya Hanga, Ngarambi, Nambondo na Mtende.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri kwa Serikali; kwanza minara ya GB3 ya TTCL Nandete, Pungutini, Chapita na Mwengei ifungwe mitambo ya GB 5/4.

Pili, vijiji vinne vya Hanga, Ngarambi, Nambondo na Mtende vipelekewe miradi ya minara ya simu za mkononi ili kumaliza changamoto ya mawasiliano ya simu za mkononi; tatu, mnara wa mawasiliano ya redio wa Nangurukuru ukamilishwe na mnara wa redio wa Mlima Kitope uboreshwe ili kuimarisha mawasiliano ya redio Kilwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne, nakuomba Mheshimiwa Waziri tuambatane pamoja tukazindue mnara mmoja wa Kipindimbi mara baadaya Mheshimiwa Rais kufanya uzinduzi wa Kitaifa wa minara 758.