Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

Hon. Edibily Kinyoma Kazala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027

MHE. EDIBILY K. KINYOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwanza ninaomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa kunijaalia kufikia siku ya leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ninamshukuru Mheshimiwa Rais tena kwa kuniteua mimi kijana mdogo hapa Bungeni kwa Wabunge wa jimbo ukiachana na wale wa Viti Maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nianze kuchangia kwa upande wa hali ya uchumi. Hali ya uchumi kwa ripoti za World Bank na pia hotuba ya Waziri Mkuu, ni ya kuridhisha hasa kwenye ukuaji wa uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, uchumi unakua kwa zaidi ya asilimia sita. Pia, hali ya umaskini inaonyesha unaelekea kupungua. Kwa ripoti ya mwisho, tulikuwa tumeshafika 26%, lakini pia, unemployment rate nayo inaonekana kwamba imepungua iko chini ya asilimia mbili nukta nane.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mazuri ambayo yanafanyika kwenye Taifa letu, nilitamani nishauri baadhi ya vitu hasa kwenye uchumi wa Taifa letu hapa. Ukiangalia kwenye ripoti kwa mujibu wa World Bank, pia na NBS (Shirika letu la Takwimu Tanzania), uchumi wetu umechangiwa kwa sehemu kubwa tatu, hasa primary activities zikiongoza zikiwa na 42.9%, lakini secondary activities zikiwa na 19.7%, lakini tertiary activities zikiwa na 37.4%.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa, kwenye shughuli hizi za msingi ambazo zinaendesha uchumi wetu, ni pamoja na kilimo na madini, hasa shughuli zinazohusisha ardhi kama resource. Mimi ninafikiri nishauri hapa. Ukiangalia kwa uchumi wetu kwa takwimu za World Bank, uchumi wa dunia ulikua kwa wastani wa asilimia tatu nukta tatu kwa mwaka 2025, lakini uchumi huu ulikuwa hasa unaongozwa na sekta hasa za teknolojia.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi uchumi wetu unaongozwa kwenye shughuli za msingi. Yaani hata ile secondary kwa maana ya manufacturing, ku-process zile raw materials, malighafi zinazotoka huko kwenye kilimo au kwenye madini, uchimbaji kule, huko inaonekana hali bado ni ndogo. Tuna 19.7% tu peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa, hii nipongeze juhudi zinazofanyika kwenye kilimo. Tunapozungumzia kilimo ni pamoja na kufungua maeneo hasa ya vijijini kwa sababu 60% kwa takwimu zilizopo wananchi wengi wanajishughulisha na kilimo. Kwa Taifa hili tuna nguvu kazi zaidi ya milioni 32. Milioni 32 hii kuna zaidi ya 97% ambayo iko kwenye informal sector. Watu hawako kwenye sekta rasmi.

Mheshimiwa Naibu Spika, yaani less than 10 percent, vijana wengi wanapata ajira kwenye formal. Maana yake tukichukua vijana ambao wana-graduate kama zaidi ya 700,000 mpaka kwenda 900,000 wanaoingia kwenye soko la ajira kila mwaka, chini ya 10% ndiyo wanaoweza kupata kwenye formal sector, lakini wengine waliobaki almost 90% plus, wote wanaenda kwenye informal sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana yake hapa ukija kwenye Taifa letu maana yake ukija tena kwenye dependency ratio inaonyesha Taifa letu bado lina utegemezi mkubwa. Yaani tuna kundi kubwa ambalo linategemea kundi dogo. Zaidi ya 80% ni kundi ambalo bado ni tegemezi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa, mapato tunayojisifia kwa Taifa hili, maana yake mapato mengi yanakusanywa na kundi dogo, lakini liko kundi kubwa ambalo halichangii chochote, pengine hatujalitambua kama sekta rasmi. Ukijumuisha bodaboda na wengine, yaani kama Taifa, bado hatujapata utambuzi rasmi wa kuwatambua kundi hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nizungumzie kwenye remittance. Kwa takwimu za World Bank bado zinaonyesha Tanzania sisi kwa Afrika Mashariki inaonekana ndiyo tunashika mkia kwa kupokea hela ndogo kutoka kwa diaspora kutoka nje ya nchi. Wameweka wazi kwamba sababu kubwa inayosababisha mpaka tunakuwa na kiasi kidogo ni gharama ya kutuma fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ndiyo tuna gharama kubwa, ni miongoni mwa nchi tatu zinazotoza kiasi kikubwa Barani Afrika. Kwa hiyo, ninafikiri kama Serikali kuna haja pia kuliangalia hili. Tupunguze gharama ili na sisi tuweze kushindana na Mataifa mengine ili watu walioko nje angalau wawe wanaweza kutuma chochote kwenye Taifa letu na sisi tuweze kunufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna issue ya consumption kwenye matumizi. Kwenye Government Consumption, matumizi ya Serikali inaonekana yanaongezeka kutoka kwenye Real GDP, lakini ukija kwenye private kwa maana ya personal, mtu mmoja mmoja inaonekana matumizi yanapungua. Mara ya mwisho inaonekana ilikuwa 3.4 percent of Real GDP.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hiki kitu nacho tena inaonyesha kwamba wananchi wa kawaida kule hali inazidi kuwa mbaya, hawana fedha mfukoni. Kwa hiyo, nini kinatokea? Maana yake pengine wananchi hawa, wengine ndio ambao wamefanya tender hawajalipwa, wengine labda wamefanya mambo fulani fulani kwa Serikali bado hawajalipwa. Kwa hiyo, kama Serikali, lazima tuangalie pia namna ya kuhakikisha wananchi wanakuwa na chochote kitu mfukoni ili consumption iweze kwenda vizuri iendane na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Serikali inakuwa na fuko la kutosha kufanya matumizi, pia watu binafsi nao wawe na fedha mfukoni za kufanya matumizi.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Malizia Mheshimiwa, muda wako umeisha.

MHE. EDIBILY K. KINYOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, okay. Kwa kumalizia, ninaomba nizungumzie issue ya NIDA na Force Account. Kwa ...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa, usianze jambo jipya, malizia tu sentensi ya mwisho.

MHE. EDIBILY K. KINYOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Wakati ninamalizia ninaomba niishauri Serikali pia iongeze issue ya suala la NIDA kwenye majimbo yetu hasa, ni changamoto kubwa sana. Kwa hiyo, Serikali ipambane.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru, ninaomba kuunga mkono hoja. (Makofi)